Ulimwengu wa kamari kuna neno wakamaria wamekua wakilitumia (the house always wins) ikiwa na maana waendeshaji wa michezo ya bahati nasibu mara zote wamekuwa wakishinda kwa namna moja ni kweli, lakini je unajua kuwa kuna matajiri wakubwa wamekuwa wachezaji wakubwa wa michezo ya bahati nasibu?
Kerry Packer anaweza kuwa mtu tajiri zaidi nchini Australia kupitia himaya ya biashara za familia yake, lakini ni mcheza kamari ambaye daima atakumbukwa. Hii ni kwa sababu Packer daima alikuwa akicheza kiasi kikubwa.

Kerry Packer anafahamika zaidi kwa uchezaji wake wa kutumia kiasi kikubwa kwenye michezo ya kasino huku akiwa amapoteza kiasi kikubwa kwenye michezo hiyo
lakini rekodi maarufu inayotambulika sana ni kiasi alichopoteza ndani ya miezi kumi takribani dola milion 40 kuanzi septemba 1999 mpaka Juni 2000 kwenye kasino za Crockford London na Bellagio Las Vegas.
Kwa bahati nzuri kwa Packer, pia alikuwa na nyakati za kufurahisha mara kwa mara. Labda mafanikio makubwa zaidi ya kamari yalikuja mwezi Mei 1995 aliposhinda dola milioni 20 ndani ya dakika 40 kwa kucheza michezo kadhaa ya blackjack yenye dau la $250,000 kwa wakati mmoja.
Watu wengi hupenda kubashiri mara kwa mara lakini kuna watu wachache ambao wamefanya michezo ya kasino kuwa kazi yao ya maisha.

Leave a Comment